JERAHA LA MOYO (02)
JERAHA LA MOYO Sehemu Ya 02 Mtunzi : Dully Tz WhatsApp : 0752747344 ILIPOISHIA..... "Hivi huyu cheupe kwani hajaona sehemu za kukaa mpaka akae kwangu sasa muache namtoa hata simuogopi" Nalson alijikaza kisabuni japo alikuwa na aibu lakini alivumilia na kumsogelea yule mwanafunzi mgeni........!!ENDELEA.... Nelson mbwembwe zote alizokuwa nazo lakini alifika pale na kujikuta amepowa ghafla baada ya macho yake kugongana na yule binti mweupe. "Am ah ila samahani kama nitakuwa nakusumbua hivi wewe ni mwanafunzi mpya kwenye darasa hili sio" Nelson aliamua tu kupotezea na kuanza kuongea mambo tofauti na aliyopanga mwanzo. "Ndiyo mimi mgeni nimekuja leo" "Ahaaa sawa ila ulifaulu hapa hapa au umeamishiwa" "Hapana nimetoka tanga nimeamishiwa hapa ila nilitakiwa niripoti jana lakini kuna dharura ilitokea sasa nimeletwa leo' "Ahaaa ok karibu mimi naitwa Nelson sijui wewe" Nelson aliongea huku akimpa mkono yule binti lakini hakutaka kupokea ...